TESDO MAKAO MAKUU TABORA

tesdo makao makuu

Usajili utafanyika kwa vituo vitatu, TABORA,DODOMA na DAR ES SALAAM, unatakiwa kudownload fomu kwenye blog ya asasi na kuijaza vyema, kisha unatakiwa ulipie ada ya uanachama na fomu kama inavyojieleza kwenye hiyo fomu. Akaunti no 01522250952400. Kwa kituo cha TABORA utakabidhi fomu yakokwa Mohamed Mapalala 0715449745, DODOMA Zahoro HM na Malale Buluba 0764492146. DAR ES SALAAM Mayasa Mzelela 0785314908, kasha baada ya muda utapatiwa risiti yako. Fomu inapatikana sehemu ya TESDO DOCUMENTS. Kwa maoni kuhusu utaratibu tuma kwenye email tesdo@rocketmail.com au simu 0716555450/0785314908.

Hamisi Masoud Mtwale

Mwenyekiti TESDO



Monday, September 3, 2012

USHAURI WA TESDO KUHUSU UPATIKANAJI WA WALIMU KATIKA SHULE ZA SEKONDARI


1.0         Taarifa fupi kuhusu program ya asasi ya kujitolea kufundisha
Awali ya yote tunapenda kuishukuru ofisi yako tukufu kwa kuwa sikivu kwa ushauri lakini pia kuchangia moja kwa moja katika kuhamasisha maendeleo ya kijamii na ya kiuchumi ya mkoa wetu wa Tabora.
Asasi yetu imeshaanza kufanya jitihada za makusudi katika kunusuru ufaulu duni wa wanafunzi wa mkoa wetu wa tabora na kwa sasa ina kambi darasa kwa ajili ya kutunga mitihani, kufanya masahihisho na kufundisha na kisha kuzifundisha mada ambazo zimeonekana kuwa ngumu kwa watahiniwa katika shule ya Itetemia na Fundikira. Pia tumeombwa na Rwanzari na tumeitikia wito kuiunganisha katika program yetu hii. Tuna walimu 22 tabora mjini na pia tuna walimu wachache Nzega na Uyui.
Pia asasi imeanza program ya kujitolea kufundisha bure (TESDO FREE TUITION) na inafanyia shule ya sekondari Kazima, tunapokea wanfunzi zaidi ya mia tano kila siku.
Mapokezi ya program zetu kwa jamii ya Tabora
Asasi imepata faraja kwa mapokezi mazuri kwa jamii ya watu wa Tabora kuhusu program yetu hii ya kujitolea kufundisha na zaidi tumefurahi shule nyingine kutuomba kufanya program hii katika shule zao mfano mzuri ni shule ya sekondari Rwanzari.

Wanafunzi na walimu wakizungumza kabla ya kuanza vipindi Kazima sekondari ,Tabora mjini

Bofya hapa kupakua taarifa yote

Sunday, August 5, 2012

WanaTESDO wakitoa huduma ya mitihani kwa wanafunzi wa Fundikira na Ruanzari






Monday, June 4, 2012

RIPOTI YA KIKAO CHA WAJUMBE WA TESDO TAREHE 03/06/2012

RIPOTI YA KIKAO CHA WAJUMBE WA TESDO TAREHE 03/06/2012 DDC MLIMANI PARK saa 10 jioni
AJENDA
  •   Ufunguzi
  •   Mradi wa kujitolea kufundisha
  •   Utafiti wa ufaulu duni wa mkoa wa Tabora,
  •   Uzinduzi wa asasi,
  •   Mengineyo
  •   Kufunga kikao. 
UFUNGUZI

Mwenyekiti alimuomba mjumbe mmoja aombe ili kufungua kikao mnamo saa kumi jioni.

MRADI WA KUJITOLEA KUFUNDISHA

Mwenyekiti alitoa maelezo ya kina kuhusu mradi huo kisha akendelea kutoa sababu au fursa za kufanya hivyo ikiwa ni pamoja na kujengea heshima mkoa, kujijengea heshima mwenyewe na kupata fursa zaidi kama hizi ambazo viongozi wakuu katika mkoa wamekuwa wakitushauri, zaidi wajumbe takribani 20 walijisajili palepale kwa ajili ya programu wakati wengine 25 wakiwa wamejisajili kwenye website, SAUTI MWANZA nao watakuwa na kikao chiniya uongozi wa coordinator wetu JOSEPH MASELE ambaye ni coordinator wa vyuo vyote jiji la Mwanza, na UDOM chini ya Zahoro HM na Malale Buluba, na SAUT TABORA chini ya CASIAN PIUS wanaendelea na usajili huo. wajumbe walipongeza kwa jinsi programu hiyo imepangwa na kuahidi ushiriki wao kwa hali yoyote kuukwamua mkoa wa Tabora na kwa kuanzia itakuwa likizo hii ya mwezi jully kisha walihimiza watu wengine waendele kujisajili il wawepo walimu wa kutosha , na kila mtu wa fani yoyote atapaswa awepo kwenye programu cha msingi tu atapewa semina ya ethics ya taaluma.Zaidi Mwenyekiti alitoa maelezo ya maaumuzi ya kamati kuhusu kuchangia nauli na kutoa t shirt za asasi kwa watakao jiunga na mradi huu wa miezi miwili na kusema kuna kiongozi kaziona jitihada zetu nae ni mkuu wetu wa mkoa FATUMA A. MWASA na kaahidi kutuchangia kuboresha harakati zetu.Wajumbe walimpongeza sana mkuu wa mkoa na kushukuru kwa uongozi wake bora na kumuona kuwa ni mkombozi wa TABORA
UTAFITI WA UFAULU DUNI WA MKOA WA TABORA

Wajumbe waipata maelezo kuwa mkuu wa mkoa ameteua TESDO na SAUT TABORA kufanya tafiti hyo juu na kuja na mpango mkakati wa kuikwamua TABORA wajumbe waliteua kamati ya kulishughulikia hilo ikiwa chini ya Dr. Almas Mabakila (MUHAS) na kupanga kuandaa project hiyo

UZINDUZI WA ASASI

Uzinduzi wa asasi mkoni umekadiliwa kufanywa mwezi wa kumi, na utasimamiwa chini ya kiongozi Frank Jackson
Ernest Minazi

...MENGINEYO

Umoja na mshikamano mpaka tuipate TABORA TUNAYOITAKA
KUFUNGA

Kikao kilifungwa kwa maombi saa 1 kasoro jioni


Wednesday, May 30, 2012

NAFASI YAKO YAKUFANYA TAFITI KATIKA MKOA WA TABOA


Monday, May 28, 2012

TAARIFA FUPI YA SEMINA


UTANGULIZI
Namshukuru Mungu kwa uwezo aliotupa Viongozi na Wana TESDO wa kuwatumikia vyema wana Tabora.Pia shukrani za dhati ziende kwa watendaji wa CG FM radio,VOT Radio na Mhe.Mstahiki Meya wa Manispaa kwa mchango wake wa TSH.50,000/=.
URATIBU WA SEMINA
Semina ya kuwaelimisha wanafunzi walio maliza kidato cha 6 na 4 iliratibiwa chini ya Uongozi wangu na wajumbe wa TESDO BW.Seifu Kazuge,Cassian Puis na Mansoor Juma tangu tarehe 21/05/2012 ofisini makao makuu Tesdo.Aidha mikamati ya kujitolea ilifanywa na majukumu kugawiwa wajumbe wote.

                                                 TESDO OFISIN-viongozi kwakiratibu Seminar

Cassian Puis alijitolea kutengeneza tangazo kwa gharama zake-TSH.100,000/=,Katibu Mtendaji nilisimamia mambo yote yahusuyo Stationaries na Seif alifuatilia Ukumbi na maandalizi yake.wajumbe wengine wakafanya zoezi ya uhamasishaji mahudhurio.
SEMINA KUFANYIKA
Mnamo tarehe 26/05/2012 saa 2.00 asubuhi wajumbe NA VIONGOZI WA TESDO waliwasili eneo la ukumbi wa SAUT/mihayo school.
Vongozi TESDO wakisubiri wajumbe wa semina-UKUMBI WA CHUO CHA SAUT TABORA
Wajumbe wa semina walitarajiwa kuwa wengi sana kwa matangazo tuliokuwa tumetoa kwa vyombo vya Redio lakini haikuwa hivyo kinyume na matarajio yetu.Lakini imani yetu ni kuwa mwanzo mgumu na harakati hizi za kubadili mitazamo na ujanja wa kutumia fursa zinazopatikana ni suala la lazima.Hali ilikuwa hivi
                       Ni wajumbe wachache sana aliohudhuria semina hii


Lakini TESDO na viongozi ake wanaamini katika harakati ya kubadili tabia na mtazamo si jambo lahisi kiasi hicho;hivyo basi kwa kuzingatia rasilimali zilizotumika kuandaa ukumbi ilitupasa kufanya semina kwa wajumbe hawa na kufikisha lengo ili tuwe na wachache wenye nguvu na sio wingi wa povu la sabuni. Semina ikaanzaa;mada zikaanza tolewa.
Mada ya kwanza: Nafasi ya wasomi kusaidia maendeleo ya Mkoa wa Tabora


Wawasilishaji mada TESDO MAKAO MAKUU-aliesimama ni SEIF(kushoto),katikati M.Mapalala na (kulia) ni mjumbe Cassian Pius.

Pamoja na hayo;mada zote zilizopangwa kuhudhurihshwa zilitolewa na wajumbe wakapata kile walicho tarajia kupata.
Mada ya pili: MFUMO WA ELIMU TANZANIA NA FURSA ZA KIELIMU.


                               Mwasilishaji: Mohamed Mapalala

Mada ya Tatu: MAISHA YA CHUO NA CHANGAMOTO ZAKE
                                Mwasilishaji: Mansoor Juma


VIBURUDISHO NA VINYWAJI :
Pamoja na umaskini tuliokuwa nao haikuwa ngumu kufanya makoo yetu safii kwa kutoa mada na kuuliza maswali;



                               wajumbe wakisikiliza mada na kuburudika soda na maji

         Meza ya wawezeshaji –TESDO MAKAO MAKUU

MCHANGANUO WA MATUMIZI
Tulipata fedha toka vyanzo vifuatavyo;

  •  Meya manispaa-50,000/=
  •  Cassian-100,000/=
  •  Mapalala 50,000/=
  •  Utawala SAUT Tabora -200,000/=

JUMLA:400,000/=

Mchanganuo huu ni kwa fedha (gharama) ila Fedha taslimu ilikuwa ni TSH.50,000/= tu.Zinginezo ni huduma zilizotolewa na wahusika kwa gharama hio.
MATUMIZI


Kutengeneza JINGO(TANGAZO)-100,000/=

  •  Kulitangaza Tangazo-30,000/=
  •  Kutoa copy na kuandaa semina papers-50,000/=
  •  Ukumbi-200,000/=
  • Soda na maji 10,000/=
MWISHO
Tunatoa tena shukrani kwa wadau wa maendeleo kufanikisha hili kwa asilimia hii ndogo.Aidha tuna amini kwa wakati mwingine tutaweza zaidi.

Taarifa hii imeandaliwa na:
KATIBU MTENDAJI –TESDO
0715449745
mapalala04@gmail.com







Thursday, May 24, 2012

Wajumbe na Viongozi wa TESDO wakiwajibika

   
  Katibu Mtendaji




      Viongozi wa tesdo wakijadili kuhusu program ya kujitolea kufundish









Wednesday, May 16, 2012

UJUMBE WA TESDO UMEMFIKIA MKUU WA MKOA WA TABORA

Tunamshukuru mungu ujumbe wa TESDO leo umemfikia mkuu wa mkoa wa TABORA, MH. FATUMA A. MWASA.
Awali ya yote tunapenda kumpongeza mama yetu kwa jitihada ambazo anaonyesha katika mkoa wetu zikiwa katika kuhamasisha maendeleo ya uchumi na jamii. Tumemueleza adhma yetu na kwa kuwa ni mdau mkuu wa maendeleo ya mkoa ametuahidi kutuunga mkono na kutuchangia kwa mradi wetu wa elimu (TESDO INITIATIVES FOR IMPROVING PERFOMANCE OF SEC SCHOOLS IN TBR REGION) na zaidi ametushauri katika NYANJA ya uchumi kuhusu miradi miwili ya KILIMO. Mwisho amewapa salam na kuwapongeza kwa kuwa na umoja huu na kuwaomba mjisajili kwa wing katika kujitolea kufundisha na katika asasi. Tena ametualika kwenye kikao kikuu cha kamati ya mkoa jumamosi tar 19/05/2012 tukashiriki na ku present. Pia tumefanikisha kupata ofisi ya makao makuu town centre.
Natoa wito kwa wote kujisajili katika asasi kwa vituo tulivyopangiana na pia kwa programu ya mwezi wa 7 ya kujitolea kufundisha. kwa usajili bofya hapa Fomu ya kujisajili kujitolea kufundisha 
Ni dhahir maendeleo yetu tutayaleta wenyewe kwa kushirikiana na wadau wengine.TESDO NI YETU, TABORA NI YETU NA MAENDELEO YAKE NI YETU PIA

Hamisi Masoud Mtwale

Mwenyekiti